,,

,,

Sunday, May 18, 2014

MATUKIO KATIKA PICHA

blogger michael monga kulia akiwa pamoja na david maeneo ya DASP  (SOKOINE UNIVERSITY OF AGRICULTURE)

Monday, May 12, 2014

PICHA MBALIMBALI ZIKIONYESHA MAENEO MBALIMBALI YA MKOA WA IRINGA KWA UPANDE WA IRINGA MJINI

ISIMILA 








MANCHESTER CITY YATWAA UBINGWA WA EPL, WAILAZA 2 – 0 WESTHAM, LIVERPOOL YAITUNGUA 2 – 1 NEWCASTLE

Manchester CityHatimaye kikosi cha Manchester City kilicho chini ya kocha mkuu ‘Manuel Pellegrini’  kimeweza   kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya England maarufu kama EPL baada ya kuibuka na ushindi wa bao 2 – 0 dhidi ya wagonga nyundo wa jiji la London Westham United katika mtanange  wa mwisho wa kufunga pazia la ligi kuu hiyo inayoongoza kwa kutazamwa na wapenzi wengi wa soka  Duniani.
PellegriniWachezaji wa Manchester City wakiwa wamemnyanyua juu kocha wao Manuel Pellegrini ikiwa ni ishara ya kuonyesha ni jinsi gani walivyokuwa na furaha
Mabao ya City yalifungwa na Samir Nasir baada ya kupewa pasi nzuri kutoka kwa  kiungo mshambuliaji Yaya Toure huku goli la pili likifungwa na Vicent Kompany. Mchezo mwingine uliokuwa wa vuta nikuvute ni ule ulioikutanisha klabu ya Liverpool waliowakaribisha nyumbani NewCastle United ambao walikubali kipigo cha bao 2 -1 kutoka kwa majogoo hao wa London  katika mtanange uliochezwa kwenye dimba la Anifield jijini humo.
Manchester City FunsMagoli ya Liverpool yalifungwa kupitia mshambuliaji wake hatari  Daniel Sturridge pamoja na Daniel Agger  aliyesawazisha huku  bao pekee la kufutia machozi kwa Newcastle likipatikana baada ya mchezaji wa Liverpool Martin Skrtel kujifunga  wakati akijaribu kuokoa mpira.
Warm welcome: The home support git right behind their team from the start of Liverpool vs Newcastle
Wachezaji wa Liverpool wakiwa wamekosa furaha licha ya ushindi wa bao 2 -1 dhidi ya NewCastle lakini haikuwa muarobani kwa Man City walioibuka mabingwa
Matokeo hayo yameiwezesha Manchester City kutwaa ubingwa huo mkubwa kwa mara ya pili ndani ya misimu mitatu wa mwaka 2011/12 pamoja na 2013/14 huku ikimaliza  kileleni mwa  ligi hiyo kwa jumla ya pointi 86,  wakati wapinzani wao wanaowafuatia ‘Liverpool’ wakiwa nyuma  yao kwa tofauti ya pointi mbil tu huku  Norwich City, Fulham pamoja na Cardiff zikijikuta zikishuka daraja.
battle cry: The Liverpool fans were in fine voice ahead of facing Newcastle in the final game of the season
mashabiki wa Liverpool wakiishangilia timu yao
Michezo mingine iliyochezwa leo ni pamoja na Cardiff iliyokubali kipigo cha bao 1 -2 toka kwa Chelsea, Fulham ikitoka sare ya 2 – 2 na Crystal Palace wakati Norwich ikiloweshwa goli 0 – 2 kutoka kwa washika mtutu wa jiji la London ‘Arsenal, Southampton ikiilzamishana sare ya bao 1 – 1 na Manchester United, Sunderland wakichezea bao 1 – 3 toka kwa Swaswea City, Tottenham Hotspurs ikiigalagaza 3 -1 Aston Villa na mwisho kabisa ni West bromwich Albion iliyopokea kipigo cha 1 – 2 toka kwa Stoke City.

Thursday, May 8, 2014

Picha:Kill Music Awards 2014 Ukumbini(Diamond aibuka kuwa kinara wa tuzo Saba,Fid Q na Weusi watamba kwenye Hip Hop)

Tuzo za Muziki za Tanzania zinazodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Lager  (KTMA2014), zilifanyika  Mei 3 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam ambapo Diamond Platinumz aliibuka kuwa mshindi wa tuzo saba.

Diamond alishinda tuzo ya Muimbaji bora wa kiume-Kizazi kipya,Video bora ya mwaka (My Number One), mtumbuizaji bora wa kiume –Kizazi kipya, Mtunzi bora wa mwaka – Kizazi Kipya, Wimbo bora wa Afro Pop, Wimbo bora wa mwaka na Wimbo bora wa kushirikiana alioshirikishwa na Nay wa Mitego (Muziki Gani).

 Angalia picha mbalimbali za washindi wa tuzo za #KTMA2014 na wasanii waliotumbuiza pamoja na watu waliohudhuria wakiwepo mastaa.



















 Angalia orodha kamili ya washindi KTMA2014:


Wimbo bora wa mwaka
Number One – Diamond 

Mwimbaji bora wa kike – kizazi kipya
Lady Jaydee

Muimbaji Bora wa kiume – Kizazi Kipya
Diamond

Muimbaji bora wa kike taarab
Isha Ramadhan

Muimbaji Bora wa kiume – Taarab
Mzee Yusuf

Muimbaji bora wa kiume – Bendi
Jose Mara

Muimbaji Bora wa Kike – bendi
Luiza Mbutu

Msanii Bora wa Hip Hop
Fid Q

Msanii Bora Chipukizi Anayechipukia
Young Killer

Rapa Bora wa Mwaka – Bendi
Furguson

Mtumbuizaji bora wa kike muziki
Isha Ramadhani

Mtumbuizaji bora wa kiume wa muziki
Diamond

Mtunzi Bora wa Mwaka – Hip Hop
Fid Q

Video Bora ya Mwaka
Number One – Diamond

Bendi ya Mwaka
Mashujaa Band

Kikundi cha Mwaka cha Taarab
Jahazi Modern Taarab

Kikundi cha mwaka cha kizazi kipya
Weusi

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka – Taarab
Enrico

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka – Kizazi kipya
Man Walter

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka – Bendi
Amoroso

Mtunzi Bora wa Mwaka – Taarab
Mzee Yusuf

Mtunzi Bora wa Mwaka – Kizazi Kipya
Diamond

Mtunzi Bora wa Mwaka – Bendi
Christian Bella

Wimbo bora wa Kiswahili – Bendi
Ushamba Mzigo – Mashujaa Band

Wimbo bora wa reggae
Niwe na Wewe – Dabo

Wimbo bora wa Afrika Mashariki
Tubonge – Jose Chameleone

Wimbo bora wa Afro Pop
Number One – Diamond

Wimbo bora wa Taarab
Wasiwasi Wako – Mzee Yusuf

Wimbo bora wa Hip Hop
Nje ya Box – Nick wa Pili f/ Joh Makini & G-Nako

Wimbo Bora wa R&B
Closer – Vanessa Mdee

Wimbo Bora wa Kushirikiana
Muziki Gani – Nay wa Mitego ft Diamond

Wimbo bora wa ragga/dancehall
Nishai – Chibwa f/ Juru

Wimbo bora wa zouk /rhumba
Yahaya – Lady Jaydee

Hall of FAME Award
Hassan Rehani Bichuka
Masoud Masoud & TBC Taifa 













source :   http://djfetty.blogspot.com/2014/05/pichakill-music-awards-2014.html