,,
AGRO-ENGINEERING
Sunday, May 18, 2014
MATUKIO KATIKA PICHA
blogger michael monga kulia akiwa pamoja na david maeneo ya DASP (SOKOINE UNIVERSITY OF AGRICULTURE)
Thursday, May 15, 2014
Tuesday, May 13, 2014
Monday, May 12, 2014
MANCHESTER CITY YATWAA UBINGWA WA EPL, WAILAZA 2 – 0 WESTHAM, LIVERPOOL YAITUNGUA 2 – 1 NEWCASTLE
Hatimaye kikosi cha Manchester City kilicho chini ya kocha mkuu ‘Manuel Pellegrini’ kimeweza kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya England maarufu kama EPL baada ya kuibuka na ushindi wa bao 2 – 0 dhidi ya wagonga nyundo wa jiji la London Westham United katika mtanange wa mwisho wa kufunga pazia la ligi kuu hiyo inayoongoza kwa kutazamwa na wapenzi wengi wa soka Duniani.
Wachezaji wa Manchester City wakiwa wamemnyanyua juu kocha wao Manuel Pellegrini ikiwa ni ishara ya kuonyesha ni jinsi gani walivyokuwa na furaha
Mabao ya City yalifungwa na Samir Nasir baada ya kupewa pasi nzuri kutoka kwa kiungo mshambuliaji Yaya Toure huku goli la pili likifungwa na Vicent Kompany. Mchezo mwingine uliokuwa wa vuta nikuvute ni ule ulioikutanisha klabu ya Liverpool waliowakaribisha nyumbani NewCastle United ambao walikubali kipigo cha bao 2 -1 kutoka kwa majogoo hao wa London katika mtanange uliochezwa kwenye dimba la Anifield jijini humo.
Magoli ya Liverpool yalifungwa kupitia mshambuliaji wake hatari Daniel Sturridge pamoja na Daniel Agger aliyesawazisha huku bao pekee la kufutia machozi kwa Newcastle likipatikana baada ya mchezaji wa Liverpool Martin Skrtel kujifunga wakati akijaribu kuokoa mpira.
Wachezaji wa Liverpool wakiwa wamekosa furaha licha ya ushindi wa bao 2 -1 dhidi ya NewCastle lakini haikuwa muarobani kwa Man City walioibuka mabingwa
Matokeo hayo yameiwezesha Manchester City kutwaa ubingwa huo mkubwa kwa mara ya pili ndani ya misimu mitatu wa mwaka 2011/12 pamoja na 2013/14 huku ikimaliza kileleni mwa ligi hiyo kwa jumla ya pointi 86, wakati wapinzani wao wanaowafuatia ‘Liverpool’ wakiwa nyuma yao kwa tofauti ya pointi mbil tu huku Norwich City, Fulham pamoja na Cardiff zikijikuta zikishuka daraja.
mashabiki wa Liverpool wakiishangilia timu yao
Michezo mingine iliyochezwa leo ni pamoja na Cardiff iliyokubali kipigo cha bao 1 -2 toka kwa Chelsea, Fulham ikitoka sare ya 2 – 2 na Crystal Palace wakati Norwich ikiloweshwa goli 0 – 2 kutoka kwa washika mtutu wa jiji la London ‘Arsenal, Southampton ikiilzamishana sare ya bao 1 – 1 na Manchester United, Sunderland wakichezea bao 1 – 3 toka kwa Swaswea City, Tottenham Hotspurs ikiigalagaza 3 -1 Aston Villa na mwisho kabisa ni West bromwich Albion iliyopokea kipigo cha 1 – 2 toka kwa Stoke City.
Thursday, May 8, 2014
Picha:Kill Music Awards 2014 Ukumbini(Diamond aibuka kuwa kinara wa tuzo Saba,Fid Q na Weusi watamba kwenye Hip Hop)
Tuzo za Muziki za Tanzania zinazodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Lager (KTMA2014), zilifanyika Mei 3 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam ambapo Diamond Platinumz aliibuka kuwa mshindi wa tuzo saba.
Angalia picha mbalimbali za washindi wa tuzo za #KTMA2014 na wasanii waliotumbuiza pamoja na watu waliohudhuria wakiwepo mastaa.
Wimbo bora wa mwaka
Number One – Diamond
Mwimbaji bora wa kike – kizazi kipya
Lady Jaydee
Muimbaji Bora wa kiume – Kizazi Kipya
Diamond
Muimbaji bora wa kike taarab
Isha Ramadhan
Muimbaji Bora wa kiume – Taarab
Mzee Yusuf
Muimbaji bora wa kiume – Bendi
Jose Mara
Muimbaji Bora wa Kike – bendi
Luiza Mbutu
Msanii Bora wa Hip Hop
Fid Q
Msanii Bora Chipukizi Anayechipukia
Young Killer
Rapa Bora wa Mwaka – Bendi
Furguson
Mtumbuizaji bora wa kike muziki
Isha Ramadhani
Mtumbuizaji bora wa kiume wa muziki
Diamond
Mtunzi Bora wa Mwaka – Hip Hop
Fid Q
Video Bora ya Mwaka
Number One – Diamond
Bendi ya Mwaka
Mashujaa Band
Kikundi cha Mwaka cha Taarab
Jahazi Modern Taarab
Kikundi cha mwaka cha kizazi kipya
Weusi
Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka – Taarab
Enrico
Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka – Kizazi kipya
Man Walter
Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka – Bendi
Amoroso
Mtunzi Bora wa Mwaka – Taarab
Mzee Yusuf
Mtunzi Bora wa Mwaka – Kizazi Kipya
Diamond
Mtunzi Bora wa Mwaka – Bendi
Christian Bella
Wimbo bora wa Kiswahili – Bendi
Ushamba Mzigo – Mashujaa Band
Wimbo bora wa reggae
Niwe na Wewe – Dabo
Wimbo bora wa Afrika Mashariki
Tubonge – Jose Chameleone
Wimbo bora wa Afro Pop
Number One – Diamond
Wimbo bora wa Taarab
Wasiwasi Wako – Mzee Yusuf
Wimbo bora wa Hip Hop
Nje ya Box – Nick wa Pili f/ Joh Makini & G-Nako
Wimbo Bora wa R&B
Closer – Vanessa Mdee
Wimbo Bora wa Kushirikiana
Muziki Gani – Nay wa Mitego ft Diamond
Wimbo bora wa ragga/dancehall
Nishai – Chibwa f/ Juru
Wimbo bora wa zouk /rhumba
Yahaya – Lady Jaydee
Hall of FAME Award
Hassan Rehani Bichuka
Masoud Masoud & TBC Taifa
Subscribe to:
Posts (Atom)